Job 3
Bible en Swahili de l’est

Dialogue entre Job et ses amis

Intervention n° 1 de Job

1 Baada ya hayo Ayubu akafunua kinywa chake, na kuilaani siku yake.
2 Ayubu akajibu, na kusema;
3 Na ipotelee mbali ile siku niliyozaliwa mimi, Na ule usiku uliosema, Mtoto mume ametungishwa mimba.
4 Siku hiyo na iwe giza; Mungu asiiangalie toka juu, Wala mwanga usiiangazie.
5 Ishikwe na giza, giza tupu, kuwa yake; Wingu na likae juu yake; Chote kiifanyacho siku kuwa giza na kiitishe.
6 Tena usiku huo, na ushikwe na giza kuu; Usihesabiwe katika siku za mwaka; Wala kutiwa katika hesabu ya miezi.
7 Tazama, usiku huo na uwe tasa; Wala isiwe ndani yake sauti ya shangwe.
8 Na waulaani hao waulaanio mchana, Hao walio tayari kumwamsha huyo lewiathani.
9 Nyota za mapambazuko yake na ziwe giza; Na utafute mwanga lakini usiupate; Wala usiyaone makope ya asubuhi;
10 Kwa sababu haukuifunga milango ya tumbo la mamangu. Wala kunifichia taabu machoni.
11 Mbona si kufa mimi tokea mimbani? Mbona nisitoe roho hapo nilipotoka tumboni?
12 Mbona hayo magoti kunipokea? Au hayo maziwa, hata nikanyonya?
13 Maana hapo ningelala na kutulia; Ningelala usingizi; na kupata kupumzika;
14 Pamoja na wafalme na washauri wa dunia, Hao waliojijengea maganjoni;
15 Au pamoja na wakuu wenye dhahabu, Waliozijaza fedha nyumba zao;
16 Au, kama kuzikwa mimba iliyoharibika, nisingekuwako; Kama wachanga wasiouona mwanga kabisa.
17 Huko waovu huacha kusumbua; Huko nako hao waliochoka wapumzika
18 Huko wafungwa waona raha pamoja; Hawaisikii sauti yake msimamizi.
19 Wakuu na wadogo wako huko; Mtumishi yu huru kwa bwana wake.
20 Mbona yeye aliye mashakani kupewa mwanga, Na hao wenye uchungu rohoni kupewa uhai;
21 Ambao wangojea mauti, lakini hawayapati; Na kuyachimbulia zaidi ya kutafuta hazina iliyostirika;
22 Ambao wafurahi mno, Na kushangilia watakapoliona kaburi?
23 Kwa nini mtu aliyezibiwa njia kupewa mwanga, Ambaye Mungu amemzingira kwa ukingo?
24 Kwani kuugua kwangu kwaja kana kwamba ni chakula, Na kunguruma kwangu kumemiminika kama maji.
25 Maana jambo hilo nichalo hunipata, Nalo linitialo hofu hunijilia.
26 Mimi sioni raha, wala situlii, wala kupumzika; Lakini huja taabu.

Introduction Bible en Swahili de l’est

Ressources bibliques

Commentaires bibliques

Un commentaire biblique éclaire la lecture de la Bible en expliquant son contexte, clarifiant les passages difficiles et enrichissant la foi. C'est essentiel pour des études bibliques approfondies, offrant une meilleure compréhension de la Parole de Dieu et des enseignements pour la vie.

Commentaires bibliques 5

Codes Strong

Les codes Strong de James Strong sont un puissant outil d'étude biblique numérant et classant les mots selon leurs origines et significations. Ils révèlent les nuances des enseignements, lient les mots apparentés entre passages, enrichissant l'interprétation et la compréhension spirituelle et historique des termes bibliques.

Codes Strong

Comparaison de traduction

Une fonction de comparaison de traduction de la Bible est un outil précieux pour les étudiants et chercheurs. Elle permet d'analyser les nuances, choix linguistiques et interprétations entre versions. Cette perspective élargit la compréhension des textes bibliques et des interprétations variées, qu'on cherche fidélité ou exploration enrichissante.

Comparer les traductions 44

Versets liés

Les versets liés révèlent des connexions profondes entre les passages bibliques, offrant une compréhension contextuelle riche et une vision globale des enseignements sacrés.

Versets liés

Dictionnaires

Le dictionnaire biblique est une ressource essentielle pour explorer en profondeur les enseignements et les significations de la Bible. Il fournit des explications claires sur les termes, les contextes historiques et les messages spirituels, permettant une meilleure compréhension des Écritures.

Dictionnaires 3