Psaumes 25
Bible en Swahili de l’est

Recherche du pardon de Dieu

1 Ee Bwana, nakuinulia nafsi yangu,
2 Ee Mungu wangu, Nimekutumaini Wewe, nisiaibike, Adui zangu wasifurahi kwa kunishinda.
3 Naam, wakungojao hawataaibika hata mmoja; Wataaibika watendao uhaini bila sababu.
4 Ee Bwana, unijulishe njia zako, Unifundishe mapito yako,
5 Uniongoze katika kweli yako, Na kunifundisha. Maana Wewe ndiwe Mungu wa wokovu wangu, Nakungoja Wewe mchana kutwa.
6 Ee Bwana, kumbuka rehema zako na fadhili zako, Maana zimekuwako tokea zamani.
7 Usiyakumbuke makosa ya ujana wangu, Wala maasi yangu. Unikumbuke kwa kadiri ya fadhili zako, Ee Bwana kwa ajili ya wema wako.
8 Bwana yu mwema, mwenye adili, Kwa hiyo atawafundisha wenye dhambi njia.
9 Wenye upole atawaongoza katika hukumu, Wenye upole atawafundisha njia yake.
10 Njia zote za Bwana ni fadhili na kweli, Kwao walishikao agano lake na shuhuda zake.
11 Ee Bwana, kwa ajili ya jina lako, Unisamehe uovu wangu, maana ni mwingi.
12 Ni nani amchaye Bwana? Atamfundisha katika njia anayoichagua.
13 Nafsi yake itakaa hali ya kufanikiwa; Wazao wake watairithi nchi.
14 Siri ya Bwana iko kwao wamchao, Naye atawajulisha agano lake.
15 Macho yangu humwelekea Bwana daima, Naye atanitoa miguu yangu katika wavu.
16 Uniangalie na kunifadhili, Maana mimi ni mkiwa na mteswa.
17 Katika shida za moyo wangu unifanyie nafasi, Na kunitoa katika dhiki zangu.
18 Utazame teso langu na taabu yangu; Unisamehe dhambi zangu zote.
19 Uwatazame adui zangu, maana ni wengi, Wananichukia kwa machukio ya ukali.
20 Unilinde nafsi yangu na kuniponya, Nisiaibike, maana nakukimbilia Wewe.
21 Ukamilifu na unyofu zinihifadhi, Maana nakungoja Wewe.
22 Ee Mungu, umkomboe Israeli, Katika taabu zake zote.

Introduction Bible en Swahili de l’est

Ressources bibliques

Commentaires bibliques

Un commentaire biblique éclaire la lecture de la Bible en expliquant son contexte, clarifiant les passages difficiles et enrichissant la foi. C'est essentiel pour des études bibliques approfondies, offrant une meilleure compréhension de la Parole de Dieu et des enseignements pour la vie.

Commentaires bibliques 5

Codes Strong

Les codes Strong de James Strong sont un puissant outil d'étude biblique numérant et classant les mots selon leurs origines et significations. Ils révèlent les nuances des enseignements, lient les mots apparentés entre passages, enrichissant l'interprétation et la compréhension spirituelle et historique des termes bibliques.

Codes Strong

Comparaison de traduction

Une fonction de comparaison de traduction de la Bible est un outil précieux pour les étudiants et chercheurs. Elle permet d'analyser les nuances, choix linguistiques et interprétations entre versions. Cette perspective élargit la compréhension des textes bibliques et des interprétations variées, qu'on cherche fidélité ou exploration enrichissante.

Comparer les traductions 44

Versets liés

Les versets liés révèlent des connexions profondes entre les passages bibliques, offrant une compréhension contextuelle riche et une vision globale des enseignements sacrés.

Versets liés

Dictionnaires

Le dictionnaire biblique est une ressource essentielle pour explorer en profondeur les enseignements et les significations de la Bible. Il fournit des explications claires sur les termes, les contextes historiques et les messages spirituels, permettant une meilleure compréhension des Écritures.

Dictionnaires 3