Job 13
Bible en Swahili de l’est

1 Tazama, jicho langu limeyaona hayo yote, Sikio langu limeyasikia na kuelewa nayo.
2 Hayo myajuayo ninyi, na mimi pia nayajua; Mimi si duni kuliko ninyi.
3 Hakika ningenena naye huyo Mwenyezi, Nami nataka kuhojiana na Mungu.
4 Lakini ninyi hubuni maneno ya uongo, Ninyi nyote ni matabibu wasiofaa.
5 Laiti mngenyamaza kabisa! Hilo lingekuwa hekima kwenu.
6 Sikieni sasa basi hoja zangu, Mkayasikie mashindano ya midomo yangu.
7 Je! Mtanena yasiyo ya haki kwa ajili ya Mungu, Na kusema kwa udanganyifu kwa ajili yake?
8 Je! Mtamwonyesha yeye upendeleo? Mtamtetea Mungu?
9 Je! Itafaa yeye kuwatafuta ninyi? Au, kama kumdanganya mtu, je! Mtamdanganya yeye?
10 Hakika atawakemea ninyi, Mkiwapendelea watu kwa siri.
11 Je! Huo ukuu wake hautawatia hofu, Na utisho wake hautawaangukia?
12 Matamko yenu ya hekima ni mithali ya majivu, Ngome zenu ni ngome za udongo.
13 Nyamazeni, niacheni, ili nipate kunena, Na hayo yatakayonijilia na yaje.
14 Nitaitwaa nyama ya mwili wangu katika meno yangu, Na kuutwaa uhai wangu mkononi mwangu!
15 Tazama, ataniua; sina tumaini; ila hata hivyonitaithibitisha njia yangu mbele yake.
16 Hili nalo litakuwa ni wokovu wangu; Kwani asiyemcha Mungu hatakaribia mbele yake.
17 Sikieni sana maneno yangu, Maelezo yangu na yaingie masikioni mwenu.
18 Angalieni sasa, nimekwisha kulitengeneza neno langu, Najua ya kuwa ni mwenye haki mimi.
19 Yuko nani atakayeshindana nami? Maana sasa nitanyamaa kimya na kutoa roho.
20 Lakini msinifanyie mambo mawili, hayo tu, Ndipo nami sitajificha usoni pako;
21 Uondoe mkono wako usinilemee; Na utisho wako usinitie hofu.
22 Basi uite wakati huo, nami nitaitika; Au, niache ninene mimi, nawe unijibu.
23 Maovu yangu na dhambi zangu ni ngapi? Nijulishe kosa langu na dhambi yangu.
24 Mbona umeuficha uso wako, Na kunihesabu kuwa ni adui yako?
25 Je! Utalitaabisha jani lipeperushwalo? Au, je! Utayafuatia hayo mabua makavu?
26 Kwani umeandika maneno ya uchungu juu yangu, Na kunirithisha maovu ya ujana wangu;
27 Waitia miguu yangu katika mkatale, na kuyaaua mapito yangu yote; Wajiandikia alama kuzizunguka nyayo za miguu yangu;
28 Nijapokuwa ni kama kitu kilichooza, kinachosinyaa, Mfano wa nguo iliyoliwa na nondo.

Introduction Bible en Swahili de l’est

Ressources bibliques

Commentaires bibliques

Un commentaire biblique éclaire la lecture de la Bible en expliquant son contexte, clarifiant les passages difficiles et enrichissant la foi. C'est essentiel pour des études bibliques approfondies, offrant une meilleure compréhension de la Parole de Dieu et des enseignements pour la vie.

Commentaires bibliques 5

Codes Strong

Les codes Strong de James Strong sont un puissant outil d'étude biblique numérant et classant les mots selon leurs origines et significations. Ils révèlent les nuances des enseignements, lient les mots apparentés entre passages, enrichissant l'interprétation et la compréhension spirituelle et historique des termes bibliques.

Codes Strong

Comparaison de traduction

Une fonction de comparaison de traduction de la Bible est un outil précieux pour les étudiants et chercheurs. Elle permet d'analyser les nuances, choix linguistiques et interprétations entre versions. Cette perspective élargit la compréhension des textes bibliques et des interprétations variées, qu'on cherche fidélité ou exploration enrichissante.

Comparer les traductions 44

Versets liés

Les versets liés révèlent des connexions profondes entre les passages bibliques, offrant une compréhension contextuelle riche et une vision globale des enseignements sacrés.

Versets liés

Dictionnaires

Le dictionnaire biblique est une ressource essentielle pour explorer en profondeur les enseignements et les significations de la Bible. Il fournit des explications claires sur les termes, les contextes historiques et les messages spirituels, permettant une meilleure compréhension des Écritures.

Dictionnaires 3