Job 19
Bible en Swahili de l’est

Intervention n° 6 de Job

1 Ndipo Ayubu akajibu, na kusema,
2 Je! Mtanichukiza nafsi yangu hata lini, Na kunivunja-vunja kwa maneno?
3 Mara kumi hizi mmenishutumu; Hamwoni haya kunifanyia mambo magumu.
4 Ingawaje nimekosa, Kosa langu hukaa kwangu mwenyewe.
5 Kwamba mtajitukuza juu yangu, Na kunena juu yangu shutumu langu;
6 Jueni basi kuwa Mungu amenipotosha, Na kunizingira kwa wavu wake.
7 Tazama, nalia, Udhalimu, lakini sisikiwi; Naulilia msaada, wala hapana hukumu.
8 Yeye ameiziba njia yangu nisipate kupita, Na kutia giza katika mapito yangu.
9 Amenivua utukufu wangu, Na kuiondoa taji kichwani mwangu.
10 Amenibomoa pande zote, nami nimetoweka; Na tumaini langu ameling’oa kama mti.
11 Tena ameziwasha ghadhabu zake juu yangu, Akanihesabia kuwa mmoja katika watesi wake.
12 Majeshi yake husongea pamoja, na kunipandishia njia yao, Na kupiga marago kuizunguka hema yangu.
13 Amewaweka ndugu zangu mbali nami, Na wanijuao wametengwa nami kabisa.
14 Watu wa mbari yangu wamekoma, Na rafiki zangu niwapendao wamenisahau.
15 Wakaao nyumbani mwangu, na vijakazi vyangu, wanihesabu kuwa mgeni; Mimi ni mgeni machoni pao.
16 Namwita mtumishi wangu, wala haniitikii, Ingawa namsihi kwa kinywa changu.
17 Pumzi zangu ni kama za mgeni kwa mke wangu, Nami ni machukizo kwa ndugu zangu.
18 Hata watoto wadogo hunidharau; Nikiondoka, huninena.
19 Wasiri wangu wote wanichukia; Na hao niliowapenda wamenigeukia.
20 Mfupa wangu unagandamana na ngozi yangu na nyama yangu, Nami nimeokoka na ngozi ya meno yangu tu.
21 Nihurumieni, nihurumieni, enyi rafiki zangu, Kwa maana mkono wa Mungu umenigusa.
22 Mbona ninyi mnaniudhi kama Mungu, Wala hamkutosheka na nyama yangu?
23 Laiti maneno yangu yangeandikwa sasa! Laiti yangeandikwa kitabuni!
24 Yakachorwa katika mwamba milele, Kwa kalamu ya chuma na risasi.
25 Lakini mimi najua ya kuwa Mteteaji wangu yu hai, Na ya kuwa hatimaye atasimama juu ya nchi.
26 Na baada ya ngozi yangu kuharibiwa hivi, Lakini, pasipokuwa na mwili wangu nitamwona Mungu;
27 Nami nitamwona mimi nafsi yangu, Na macho yangu yatamtazama, wala si mwingine. Mtima wangu unazimia ndani yangu.
28 Kama mkisema, Jinsi tutakavyomwudhi! Kwa kuwa shina la jambo hili limeonekana kwake;
29 Uogopeni upanga; Kwa maana adhabu za upanga zina ghadhabu, Mpate kujua ya kwamba hukumu iko.

Introduction Bible en Swahili de l’est

Ressources bibliques

Commentaires bibliques

Un commentaire biblique éclaire la lecture de la Bible en expliquant son contexte, clarifiant les passages difficiles et enrichissant la foi. C'est essentiel pour des études bibliques approfondies, offrant une meilleure compréhension de la Parole de Dieu et des enseignements pour la vie.

Commentaires bibliques 5

Codes Strong

Les codes Strong de James Strong sont un puissant outil d'étude biblique numérant et classant les mots selon leurs origines et significations. Ils révèlent les nuances des enseignements, lient les mots apparentés entre passages, enrichissant l'interprétation et la compréhension spirituelle et historique des termes bibliques.

Codes Strong

Comparaison de traduction

Une fonction de comparaison de traduction de la Bible est un outil précieux pour les étudiants et chercheurs. Elle permet d'analyser les nuances, choix linguistiques et interprétations entre versions. Cette perspective élargit la compréhension des textes bibliques et des interprétations variées, qu'on cherche fidélité ou exploration enrichissante.

Comparer les traductions 45

Versets liés

Les versets liés révèlent des connexions profondes entre les passages bibliques, offrant une compréhension contextuelle riche et une vision globale des enseignements sacrés.

Versets liés

Dictionnaires

Le dictionnaire biblique est une ressource essentielle pour explorer en profondeur les enseignements et les significations de la Bible. Il fournit des explications claires sur les termes, les contextes historiques et les messages spirituels, permettant une meilleure compréhension des Écritures.

Dictionnaires 3