Théo place, étudier sérieusement la parole
Tous droits réservés
© Théo place - 2023

Job 19
Versets liés

Intervention n° 6 de Job

1 Ndipo Ayubu akajibu, na kusema,
2 Je! Mtanichukiza nafsi yangu hata lini, Na kunivunja-vunja kwa maneno?
3 Mara kumi hizi mmenishutumu; Hamwoni haya kunifanyia mambo magumu.
4 Ingawaje nimekosa, Kosa langu hukaa kwangu mwenyewe.
5 Kwamba mtajitukuza juu yangu, Na kunena juu yangu shutumu langu;
6 Jueni basi kuwa Mungu amenipotosha, Na kunizingira kwa wavu wake.
7 Tazama, nalia, Udhalimu, lakini sisikiwi; Naulilia msaada, wala hapana hukumu.
8 Yeye ameiziba njia yangu nisipate kupita, Na kutia giza katika mapito yangu.
9 Amenivua utukufu wangu, Na kuiondoa taji kichwani mwangu.
10 Amenibomoa pande zote, nami nimetoweka; Na tumaini langu ameling’oa kama mti.
11 Tena ameziwasha ghadhabu zake juu yangu, Akanihesabia kuwa mmoja katika watesi wake.
12 Majeshi yake husongea pamoja, na kunipandishia njia yao, Na kupiga marago kuizunguka hema yangu.
13 Amewaweka ndugu zangu mbali nami, Na wanijuao wametengwa nami kabisa.
14 Watu wa mbari yangu wamekoma, Na rafiki zangu niwapendao wamenisahau.
15 Wakaao nyumbani mwangu, na vijakazi vyangu, wanihesabu kuwa mgeni; Mimi ni mgeni machoni pao.
16 Namwita mtumishi wangu, wala haniitikii, Ingawa namsihi kwa kinywa changu.
17 Pumzi zangu ni kama za mgeni kwa mke wangu, Nami ni machukizo kwa ndugu zangu.
18 Hata watoto wadogo hunidharau; Nikiondoka, huninena.
19 Wasiri wangu wote wanichukia; Na hao niliowapenda wamenigeukia.
20 Mfupa wangu unagandamana na ngozi yangu na nyama yangu, Nami nimeokoka na ngozi ya meno yangu tu.
21 Nihurumieni, nihurumieni, enyi rafiki zangu, Kwa maana mkono wa Mungu umenigusa.
22 Mbona ninyi mnaniudhi kama Mungu, Wala hamkutosheka na nyama yangu?
23 Laiti maneno yangu yangeandikwa sasa! Laiti yangeandikwa kitabuni!
24 Yakachorwa katika mwamba milele, Kwa kalamu ya chuma na risasi.
25 Lakini mimi najua ya kuwa Mteteaji wangu yu hai, Na ya kuwa hatimaye atasimama juu ya nchi.
26 Na baada ya ngozi yangu kuharibiwa hivi, Lakini, pasipokuwa na mwili wangu nitamwona Mungu;
27 Nami nitamwona mimi nafsi yangu, Na macho yangu yatamtazama, wala si mwingine. Mtima wangu unazimia ndani yangu.
28 Kama mkisema, Jinsi tutakavyomwudhi! Kwa kuwa shina la jambo hili limeonekana kwake;
29 Uogopeni upanga; Kwa maana adhabu za upanga zina ghadhabu, Mpate kujua ya kwamba hukumu iko.

Introduction de la Bible en Swahili de l’est

Verset liés

L'outil de verset lié est un instrument précieux qui ouvre des horizons nouveaux dans l'étude biblique. En reliant les versets apparentés au sein des Écritures, cet outil permet aux chercheurs et aux étudiants de la Bible d'explorer les thèmes, les concepts et les enseignements clés à travers différents livres bibliques. Grâce à la fonctionnalité de verset lié, nous pouvons établir des connexions profondes entre les passages, obtenir une compréhension contextuelle plus profonde et saisir la cohérence et la richesse des enseignements bibliques dans leur ensemble. Que ce soit pour des études personnelles, des enseignements ou des recherches plus poussées, l'outil de verset lié s'avère être un compagnon précieux qui enrichit notre exploration des vérités bibliques et renforce notre compréhension globale des Écritures saintes.