Job 27
Bible en Swahili de l’est

Conclusion de Job

1 Kisha Ayubu akaendelea na mithali yake, na kusema,
2 Kama aishivyo Mungu, aliyeniondolea haki yangu; Huyo Mwenyezi aliyeitesa nafsi yangu;
3 (Kwa kuwa uhai wangu ukali mzima ndani yangu, Na roho ya Mungu i katika pua yangu;)
4 Hakika midomo yangu haitanena yasiyo haki, Wala ulimi wangu hautatamka udanganyifu.
5 Hasha! Nisiwahesabie ninyi kuwa na haki; Hata nitakapokufa sitajiondolea uelekevu wangu.
6 Haki yangu naishika sana, wala sitaiacha; Moyo wangu hautanisuta wakati nikiwapo hai.
7 Adui yangu na awe kama huyo mwovu, Na mwenye kuondoka kinyume changu na awe kama asiye haki.
8 Kwani tumaini la mpotovu ni nini, ingawa ajipatia faida, Hapo Mungu amwondoleapo roho yake?
9 Je! Mungu atakisikia kilio chake, Taabu zitakapomfikilia?
10 Je! Atajifurahisha katika Mwenyezi, Na kumlingana Mungu nyakati zote?
11 Nitawafundisha ninyi mambo ya mkono wa Mungu; Hayo yaliyo kwa Mwenyezi sitayaficha.
12 Tazama, ninyi nyote mmeyaona wenyewe; Mbona basi mmebatilika kabisa?
13 Hii ndiyo sehemu ya mtu mwovu kwa Mungu, Na urithi wa hao waoneao, waupokeao kwa Mwenyezi.
14 Watoto wake wakiongezeka ni kwa upanga; Na wazao wake hawatashiba chakula.
15 Hao watakaosalia kwake watazikwa katika kufa, Wala wajane wake waliofiwa na waume hawataomboleza.
16 Ajapokusanya fedha kama mavumbi, Na kujifanyia mavazi kama udongo kwa wingi;
17 Yumkini kuyatengeza, lakini wenye haki watayavaa, Nao wasio na hatia watazigawanya hizo fedha.
18 Yeye hujenga nyumba yake kama mdudu, Na kama kibanda afanyacho mlinzi.
19 Yeye hujilaza hali ni tajiri, lakini ndio mwisho; Hufunua macho yake, naye hayuko.
20 Vitisho vyampata kama maji mengi; Dhoruba humwiba usiku.
21 Upepo wa mashariki humchukua, naye huondoka; Na kumkumba atoke mahali pake.
22 Kwani Mungu atamtupia asimhurumie; Angependa kuukimbia mkono wake.
23 Watu watampigia makofi, Na kumzomea atoke mahali pake.

Introduction Bible en Swahili de l’est

Ressources bibliques

Commentaires bibliques

Un commentaire biblique éclaire la lecture de la Bible en expliquant son contexte, clarifiant les passages difficiles et enrichissant la foi. C'est essentiel pour des études bibliques approfondies, offrant une meilleure compréhension de la Parole de Dieu et des enseignements pour la vie.

Commentaires bibliques 5

Codes Strong

Les codes Strong de James Strong sont un puissant outil d'étude biblique numérant et classant les mots selon leurs origines et significations. Ils révèlent les nuances des enseignements, lient les mots apparentés entre passages, enrichissant l'interprétation et la compréhension spirituelle et historique des termes bibliques.

Codes Strong

Comparaison de traduction

Une fonction de comparaison de traduction de la Bible est un outil précieux pour les étudiants et chercheurs. Elle permet d'analyser les nuances, choix linguistiques et interprétations entre versions. Cette perspective élargit la compréhension des textes bibliques et des interprétations variées, qu'on cherche fidélité ou exploration enrichissante.

Comparer les traductions 44

Versets liés

Les versets liés révèlent des connexions profondes entre les passages bibliques, offrant une compréhension contextuelle riche et une vision globale des enseignements sacrés.

Versets liés

Dictionnaires

Le dictionnaire biblique est une ressource essentielle pour explorer en profondeur les enseignements et les significations de la Bible. Il fournit des explications claires sur les termes, les contextes historiques et les messages spirituels, permettant une meilleure compréhension des Écritures.

Dictionnaires 3