Psaumes 107
Bible en Swahili de l’est

Cinquième livre

La grâce divine

1 Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema, Kwa maana fadhili zake ni za milele.
2 Na waseme hivi waliokombolewa na Bwana, Wale aliowakomboa na mkono wa mtesi.
3 Akawakusanya kutoka nchi zote, Mashariki na magharibi, kaskazini na kusini.
4 Walitanga-tanga jangwani katika njia ya nyika; Hawakuona mji wa kukaa.
5 Waliona njaa, waliona na kiu, Nafsi yao ilikuwa ikizimia ndani yao.
6 Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao.
7 Akawaongoza kwa njia ya kunyoka, Wapate kwenda mpaka mji wa kukaa.
8 Na wamshukuru Bwana, kwa fadhili zake, Na maajabu yake kwa wanadamu.
9 Maana hushibisha nafsi yenye shauku, Na nafsi yenye njaa huijaza mema.
10 Waliokaa katika giza na uvuli wa mauti, Wamefungwa katika taabu na chuma,
11 Kwa sababu waliyaasi maneno ya Mungu, Wakalidharau shauri lake Aliye juu.
12 Hata akawadhili moyo kwa taabu, Wakajikwaa wala hakuna msaidizi.
13 Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao.
14 Aliwatoa katika giza na uvuli wa mauti, Akayavunja mafungo yao.
15 Na wamshukuru Bwana kwa fadhili zake, Na maajabu yake kwa wanadamu.
16 Maana ameivunja milango ya shaba, Ameyakata mapingo ya chuma.
17 Wapumbavu, kwa sababu ya ukosaji wao, Na kwa sababu ya maovu yao, hujitesa.
18 Nafsi zao zachukia kila namna ya chakula, Wameyakaribia malango ya mauti.
19 Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao.
20 Hulituma neno lake, huwaponya, Huwatoa katika maangamizo yao.
21 Na wamshukuru Bwana kwa fadhili zake, Na maajabu yake kwa wanadamu.
22 Na wamtolee dhabihu za kushukuru, Na kuyasimulia matendo yake kwa kuimba.
23 Washukao baharini katika merikebu, Wafanyao kazi yao katika maji mengi,
24 Hao huziona kazi za Bwana, Na maajabu yake vilindini.
25 Maana husema, akavumisha upepo wa dhoruba, Ukayainua juu mawimbi yake.
26 Wapanda mbinguni, watelemka vilindini, Nafsi yao yayeyuka kwa hali mbaya.
27 Wayumba-yumba, wapepesuka kama mlevi, Akili zao zote zawapotea.
28 Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao.
29 Huituliza dhoruba, ikawa shwari, Mawimbi yake yakanyamaza.
30 Ndipo walipofurahi kwa kuwa yametulia Naye huwaleta mpaka bandari waliyoitamani.
31 Na wamshukuru Bwana kwa fadhili zake, Na maajabu yake kwa wanadamu.
32 Na wamtukuze katika kusanyiko la watu, Na wamhimidi katika baraza ya wazee.
33 Amegeuza mito ikawa jangwa, Na chemchemi za maji zikawa nchi ya kiu.
34 Nchi ya matunda mengi ikawa uwanda wa chumvi, Kwa sababu ya ubaya wao walioikaa.
35 Amegeuza jangwa ikawa ziwa la maji, Na nchi kavu ikawa chemchemi za maji.
36 Maana amewakalisha huko wenye njaa, Nao wametengeneza mji wa kukaa.
37 Wakapanda mbegu katika mashamba, Na kutia mizabibu iliyotoa matunda yake.
38 Naye huwabariki wakaongezeka sana, Wala hayapunguzi makundi yao.
39 Kisha wakapungua na kudhilika, Kwa kuonewa na mabaya na huzuni.
40 Akawamwagia wakuu dharau, Na kuwazungusha katika nyika isiyo na njia.
41 Akamweka mhitaji juu mbali na mateso, Akamfanyia jamaa kama kundi la kondoo.
42 Wanyofu wa moyo wataona na kufurahi, Na uovu wa kila namna utajifumba kinywa.
43 Aliye na hekima na ayaangalie hayo; Na wazitafakari fadhili za Bwana.

Introduction Bible en Swahili de l’est

Ressources bibliques

Commentaires bibliques

Un commentaire biblique éclaire la lecture de la Bible en expliquant son contexte, clarifiant les passages difficiles et enrichissant la foi. C'est essentiel pour des études bibliques approfondies, offrant une meilleure compréhension de la Parole de Dieu et des enseignements pour la vie.

Commentaires bibliques 5

Codes Strong

Les codes Strong de James Strong sont un puissant outil d'étude biblique numérant et classant les mots selon leurs origines et significations. Ils révèlent les nuances des enseignements, lient les mots apparentés entre passages, enrichissant l'interprétation et la compréhension spirituelle et historique des termes bibliques.

Codes Strong

Comparaison de traduction

Une fonction de comparaison de traduction de la Bible est un outil précieux pour les étudiants et chercheurs. Elle permet d'analyser les nuances, choix linguistiques et interprétations entre versions. Cette perspective élargit la compréhension des textes bibliques et des interprétations variées, qu'on cherche fidélité ou exploration enrichissante.

Comparer les traductions 44

Versets liés

Les versets liés révèlent des connexions profondes entre les passages bibliques, offrant une compréhension contextuelle riche et une vision globale des enseignements sacrés.

Versets liés

Dictionnaires

Le dictionnaire biblique est une ressource essentielle pour explorer en profondeur les enseignements et les significations de la Bible. Il fournit des explications claires sur les termes, les contextes historiques et les messages spirituels, permettant une meilleure compréhension des Écritures.

Dictionnaires 3