Psaumes 118
Bible en Swahili de l’est

Louange à Dieu pour sa bonté

1 Haleluya. Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema, Kwa maana fadhili zake ni za milele.
2 Israeli na aseme sasa, Ya kwamba fadhili zake ni za milele.
3 Mlango wa Haruni na waseme sasa, Ya kwamba fadhili zake ni za milele.
4 Wamchao Bwana na waseme sasa, Ya kwamba fadhili zake ni za milele.
5 Katika shida yangu nalimwita Bwana; Bwana akanijibu akaniweka panapo nafasi.
6 Bwana yuko upande wangu, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini?
7 Bwana yuko upande wangu, msaidizi wangu, Kwa hiyo nitawaona wanaonichukia wameshindwa.
8 Ni heri kumkimbilia Bwana Kuliko kuwatumainia wanadamu.
9 Ni heri kumkimbilia Bwana. Kuliko kuwatumainia wakuu.
10 Mataifa yote walinizunguka; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
11 Walinizunguka, naam, walinizunguka; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
12 Walinizunguka kama nyuki, Walizimika kama moto wa miibani; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.
13 Ulinisukuma sana ili nianguke; Lakini Bwana akanisaidia.
14 Bwana ni nguvu zangu na wimbo wangu, Naye amekuwa wokovu wangu.
15 Sauti ya furaha na wokovu Imo hemani mwao wenye haki; Mkono wa kuume wa Bwana hutenda makuu.
16 Mkono wa kuume wa Bwana umetukuzwa; Mkono wa kuume wa Bwana hutenda makuu.
17 Sitakufa bali nitaishi, Nami nitayasimulia matendo ya Bwana.
18 Bwana ameniadhibu sana, Lakini hakuniacha nife.
19 Nifungulieni malango ya haki, Nitaingia na kumshukuru Bwana.
20 Lango hili ni la Bwana, Wenye haki ndio watakaoliingia.
21 Nitakushukuru kwa maana umenijibu, Nawe umekuwa wokovu wangu.
22 Jiwe walilolikataa waashi Limekuwa jiwe kuu la pembeni.
23 Neno hili limetoka kwa Bwana, Nalo ni ajabu machoni petu.
24 Siku hii ndiyo aliyoifanya Bwana, Tutashangilia na kuifurahia.
25 Ee Bwana, utuokoe, twakusihi; Ee Bwana, utufanikishe, twakusihi.
26 Na abarikiwe yeye ajaye kwa jina la Bwana; Tumewabarikia toka nyumbani mwa Bwana.
27 Bwana ndiye aliye Mungu, Naye ndiye aliyetupa nuru. Ifungeni dhabihu kwa kamba Pembeni mwa madhabahu.
28 Ndiwe Mungu wangu, nami nitakushukuru, Ndiwe Mungu wangu, nami nitakutukuza.
29 Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema, Kwa maana fadhili zake ni za milele.

Introduction Bible en Swahili de l’est

Ressources bibliques

Commentaires bibliques

Un commentaire biblique éclaire la lecture de la Bible en expliquant son contexte, clarifiant les passages difficiles et enrichissant la foi. C'est essentiel pour des études bibliques approfondies, offrant une meilleure compréhension de la Parole de Dieu et des enseignements pour la vie.

Commentaires bibliques 5

Codes Strong

Les codes Strong de James Strong sont un puissant outil d'étude biblique numérant et classant les mots selon leurs origines et significations. Ils révèlent les nuances des enseignements, lient les mots apparentés entre passages, enrichissant l'interprétation et la compréhension spirituelle et historique des termes bibliques.

Codes Strong

Comparaison de traduction

Une fonction de comparaison de traduction de la Bible est un outil précieux pour les étudiants et chercheurs. Elle permet d'analyser les nuances, choix linguistiques et interprétations entre versions. Cette perspective élargit la compréhension des textes bibliques et des interprétations variées, qu'on cherche fidélité ou exploration enrichissante.

Comparer les traductions 44

Versets liés

Les versets liés révèlent des connexions profondes entre les passages bibliques, offrant une compréhension contextuelle riche et une vision globale des enseignements sacrés.

Versets liés

Dictionnaires

Le dictionnaire biblique est une ressource essentielle pour explorer en profondeur les enseignements et les significations de la Bible. Il fournit des explications claires sur les termes, les contextes historiques et les messages spirituels, permettant une meilleure compréhension des Écritures.

Dictionnaires 3