Psaumes 25
Comparer les traductions

Recherche du pardon de Dieu

1 Ee Bwana, nakuinulia nafsi yangu,
2 Ee Mungu wangu, Nimekutumaini Wewe, nisiaibike, Adui zangu wasifurahi kwa kunishinda.
3 Naam, wakungojao hawataaibika hata mmoja; Wataaibika watendao uhaini bila sababu.
4 Ee Bwana, unijulishe njia zako, Unifundishe mapito yako,
5 Uniongoze katika kweli yako, Na kunifundisha. Maana Wewe ndiwe Mungu wa wokovu wangu, Nakungoja Wewe mchana kutwa.
6 Ee Bwana, kumbuka rehema zako na fadhili zako, Maana zimekuwako tokea zamani.
7 Usiyakumbuke makosa ya ujana wangu, Wala maasi yangu. Unikumbuke kwa kadiri ya fadhili zako, Ee Bwana kwa ajili ya wema wako.
8 Bwana yu mwema, mwenye adili, Kwa hiyo atawafundisha wenye dhambi njia.
9 Wenye upole atawaongoza katika hukumu, Wenye upole atawafundisha njia yake.
10 Njia zote za Bwana ni fadhili na kweli, Kwao walishikao agano lake na shuhuda zake.
11 Ee Bwana, kwa ajili ya jina lako, Unisamehe uovu wangu, maana ni mwingi.
12 Ni nani amchaye Bwana? Atamfundisha katika njia anayoichagua.
13 Nafsi yake itakaa hali ya kufanikiwa; Wazao wake watairithi nchi.
14 Siri ya Bwana iko kwao wamchao, Naye atawajulisha agano lake.
15 Macho yangu humwelekea Bwana daima, Naye atanitoa miguu yangu katika wavu.
16 Uniangalie na kunifadhili, Maana mimi ni mkiwa na mteswa.
17 Katika shida za moyo wangu unifanyie nafasi, Na kunitoa katika dhiki zangu.
18 Utazame teso langu na taabu yangu; Unisamehe dhambi zangu zote.
19 Uwatazame adui zangu, maana ni wengi, Wananichukia kwa machukio ya ukali.
20 Unilinde nafsi yangu na kuniponya, Nisiaibike, maana nakukimbilia Wewe.
21 Ukamilifu na unyofu zinihifadhi, Maana nakungoja Wewe.
22 Ee Mungu, umkomboe Israeli, Katika taabu zake zote.

Introduction de la Bible en Swahili de l’est

Ressources

Commentaires bibliques

Un commentaire biblique enrichit la lecture de la Bible en fournissant des explications historiques, contextuelles et spirituelles. Il clarifie les passages complexes, ouvre de nouvelles perspectives d'interprétation et renforce votre compréhension de la foi. Cet outil est essentiel pour les études bibliques approfondies, aidant les croyants à mieux saisir la Parole de Dieu et à en tirer des leçons significatives pour leur vie.

comparaison de traduction

Une fonction de comparaison de traduction de la Bible est un outil puissant pour les étudiants de la Bible et les chercheurs. Elle permet de comparer différentes versions de la Bible pour comprendre les nuances de traduction, les choix linguistiques et les interprétations. Cette fonction offre une perspective élargie sur les textes bibliques, aidant à saisir la diversité des interprétations possibles. Que vous cherchiez une traduction plus fidèle aux originaux ou souhaitiez explorer les différences pour enrichir votre compréhension, cette fonction vous offre une meilleure perspective sur les Écritures sacrées.

Pour commencer à utliser ces outils il vous suffit de cliquer sur les catégories ci-dessus.