Proverbes 6
Comparer les traductions

Le danger de se porter garant

1 Mwanangu, kama umekuwa mdhamini wa rafiki yako, Ikiwa wewe na mgeni mmepana mikono,
2 Basi umetegwa kwa maneno ya kinywa chako, Umekamatwa kwa maneno ya kinywa chako,
3 Sasa, mwanangu, fanya hivi ukajiokoe, Kwa kuwa umejitia mkononi mwa jirani yako; Nenda ukanyenyekee, na kumsihi jirani yako.
4 Usiache macho yako kupata usingizi, Wala kope za macho yako kusinzia.
5 Ujiponye kama paa na mkono wa mwindaji, Na kama ndege katika mkono wa mtega mitego.

La paresse

6 Ewe mvivu, mwendee chungu, Zitafakari njia zake ukapate hekima.
7 Kwa maana yeye hana akida, Wala msimamizi, wala mkuu,
8 Lakini hujiwekea akiba ya chakula wakati wa jua; Hukusanya chakula chake wakati wa mavuno.
9 Ewe mvivu, utalala hata lini? Utaondoka lini katika usingizi wako?
10 Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, Bado kukunja mikono upate usingizi!
11 Hivyo umaskini wako huja kama mnyang’anyi, Na uhitaji wako kama mtu mwenye silaha.

L’homme double

12 Mtu asiyefaa kitu, mtu wa uovu; Huenda njiani mwenye kinywa cha upotofu.
13 Hukonyeza kwa macho, hunena kwa miguu, Huwaashiria watu kwa vidole vyake.
14 Mna upotofu moyoni mwake, hutunga uovu daima, Hupanda mbegu za magomvi.
15 Basi msiba utampata kwa ghafula; Ghafula atavunjika, bila njia ya kupona.
16 Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana; Naam, viko saba vilivyo chukizo kwake.
17 Macho ya kiburi, ulimi wa uongo, Na mikono imwagayo damu isiyo na hatia;
18 Moyo uwazao mawazo mabaya; Miguu iliyo myepesi kukimbilia maovu;
19 Shahidi wa uongo asemaye uongo; Naye apandaye mbegu za fitina kati ya ndugu.

Les conséquences de l’adultère

20 Mwanangu, shika maagizo ya baba yako, Wala usiiache sheria ya mama yako.
21 Yafunge hayo katika moyo wako daima; Jivike hayo shingoni mwako.
22 Uendapo yatakuongoza, ulalapo yatakulinda, Na uamkapo yatazungumza nawe.
23 Maana maagizo hayo ni taa, na sheria hiyo ni nuru, Na maonyo ya kumwadilisha mtu ni njia ya uzima.
24 Yakulinde na mwanamke mwovu, asikupate, Na kukuponya na ubembelezi wa mgeni.
25 Usiutamani uzuri wake moyoni mwako; Wala usikubali akunase kwa kope za macho yake.
26 Maana kwa malaya mtu hutiwa katika hali ya kuhitaji kipande cha mkate; Na kahaba humwinda mtu anase nafsi yake iliyo ya thamani
27 Je! Mtu aweza kuua moto kifuani pake, Na nguo zake zisiteketezwe?
28 Je! Mtu aweza kukanyaga makaa ya moto, Na nyayo zake zisiungue?
29 Ndivyo alivyo aingiaye kwa mke wa jirani yake; Kila mtu amgusaye huyo atakuwa na hatia.
30 Watu hawamdharau mwivi, Akiiba ili kujishibisha, iwapo aona njaa;
31 Lakini akipatikana, atalipa mara saba; Atatoa mali yote ya nyumba yake.
32 Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake.
33 Atapata jeraha na kuvunjiwa heshima; Wala fedheha yake haitafutika.
34 Maana wivu ni ghadhabu ya mtu; Wala hatahurumia siku ya kujilipiza kisasi.
35 Hatakubali ukombozi uwao wote; Wala hatakuwa radhi, ujapomlipa vitu vingi.

Introduction de la Bible en Swahili de l’est

Ressources

Commentaires bibliques

Un commentaire biblique enrichit la lecture de la Bible en fournissant des explications historiques, contextuelles et spirituelles. Il clarifie les passages complexes, ouvre de nouvelles perspectives d'interprétation et renforce votre compréhension de la foi. Cet outil est essentiel pour les études bibliques approfondies, aidant les croyants à mieux saisir la Parole de Dieu et à en tirer des leçons significatives pour leur vie.

comparaison de traduction

Une fonction de comparaison de traduction de la Bible est un outil puissant pour les étudiants de la Bible et les chercheurs. Elle permet de comparer différentes versions de la Bible pour comprendre les nuances de traduction, les choix linguistiques et les interprétations. Cette fonction offre une perspective élargie sur les textes bibliques, aidant à saisir la diversité des interprétations possibles. Que vous cherchiez une traduction plus fidèle aux originaux ou souhaitiez explorer les différences pour enrichir votre compréhension, cette fonction vous offre une meilleure perspective sur les Écritures sacrées.

Pour commencer à utliser ces outils il vous suffit de cliquer sur les catégories ci-dessus.