Job 3
Comparer les traductions

Dialogue entre Job et ses amis

Intervention n° 1 de Job

1 Baada ya hayo Ayubu akafunua kinywa chake, na kuilaani siku yake.
2 Ayubu akajibu, na kusema;
3 Na ipotelee mbali ile siku niliyozaliwa mimi, Na ule usiku uliosema, Mtoto mume ametungishwa mimba.
4 Siku hiyo na iwe giza; Mungu asiiangalie toka juu, Wala mwanga usiiangazie.
5 Ishikwe na giza, giza tupu, kuwa yake; Wingu na likae juu yake; Chote kiifanyacho siku kuwa giza na kiitishe.
6 Tena usiku huo, na ushikwe na giza kuu; Usihesabiwe katika siku za mwaka; Wala kutiwa katika hesabu ya miezi.
7 Tazama, usiku huo na uwe tasa; Wala isiwe ndani yake sauti ya shangwe.
8 Na waulaani hao waulaanio mchana, Hao walio tayari kumwamsha huyo lewiathani.
9 Nyota za mapambazuko yake na ziwe giza; Na utafute mwanga lakini usiupate; Wala usiyaone makope ya asubuhi;
10 Kwa sababu haukuifunga milango ya tumbo la mamangu. Wala kunifichia taabu machoni.
11 Mbona si kufa mimi tokea mimbani? Mbona nisitoe roho hapo nilipotoka tumboni?
12 Mbona hayo magoti kunipokea? Au hayo maziwa, hata nikanyonya?
13 Maana hapo ningelala na kutulia; Ningelala usingizi; na kupata kupumzika;
14 Pamoja na wafalme na washauri wa dunia, Hao waliojijengea maganjoni;
15 Au pamoja na wakuu wenye dhahabu, Waliozijaza fedha nyumba zao;
16 Au, kama kuzikwa mimba iliyoharibika, nisingekuwako; Kama wachanga wasiouona mwanga kabisa.
17 Huko waovu huacha kusumbua; Huko nako hao waliochoka wapumzika
18 Huko wafungwa waona raha pamoja; Hawaisikii sauti yake msimamizi.
19 Wakuu na wadogo wako huko; Mtumishi yu huru kwa bwana wake.
20 Mbona yeye aliye mashakani kupewa mwanga, Na hao wenye uchungu rohoni kupewa uhai;
21 Ambao wangojea mauti, lakini hawayapati; Na kuyachimbulia zaidi ya kutafuta hazina iliyostirika;
22 Ambao wafurahi mno, Na kushangilia watakapoliona kaburi?
23 Kwa nini mtu aliyezibiwa njia kupewa mwanga, Ambaye Mungu amemzingira kwa ukingo?
24 Kwani kuugua kwangu kwaja kana kwamba ni chakula, Na kunguruma kwangu kumemiminika kama maji.
25 Maana jambo hilo nichalo hunipata, Nalo linitialo hofu hunijilia.
26 Mimi sioni raha, wala situlii, wala kupumzika; Lakini huja taabu.

Introduction de la Bible en Swahili de l’est

Ressources

Commentaires bibliques

Un commentaire biblique enrichit la lecture de la Bible en fournissant des explications historiques, contextuelles et spirituelles. Il clarifie les passages complexes, ouvre de nouvelles perspectives d'interprétation et renforce votre compréhension de la foi. Cet outil est essentiel pour les études bibliques approfondies, aidant les croyants à mieux saisir la Parole de Dieu et à en tirer des leçons significatives pour leur vie.

comparaison de traduction

Une fonction de comparaison de traduction de la Bible est un outil puissant pour les étudiants de la Bible et les chercheurs. Elle permet de comparer différentes versions de la Bible pour comprendre les nuances de traduction, les choix linguistiques et les interprétations. Cette fonction offre une perspective élargie sur les textes bibliques, aidant à saisir la diversité des interprétations possibles. Que vous cherchiez une traduction plus fidèle aux originaux ou souhaitiez explorer les différences pour enrichir votre compréhension, cette fonction vous offre une meilleure perspective sur les Écritures sacrées.

Pour commencer à utliser ces outils il vous suffit de cliquer sur les catégories ci-dessus.