Proverbes 5
Versets liés

L’adultère

1 Mwanangu, sikiliza hekima yangu; Tega sikio lako, mzisikie akili zangu;
2 Upate kuilinda busara, Na midomo yako iyahifadhi maarifa.
3 Maana midomo ya malaya hudondoza asali, Na kinywa chake ni laini kuliko mafuta;
4 Lakini mwisho wake ni mchungu kuliko pakanga; Ni mkali kama upanga wa makali kuwili.
5 Miguu yake inatelemkia mauti; Hatua zake zinashikamana na kuzimu;
6 Hata asiweze kuiona njia sawa ya uzima; Njia zake ni za kutanga-tanga wala hana habari.
7 Basi, wanangu, nisikilizeni sasa, Wala msiache maneno ya kinywa changu.
8 Itenge njia yako mbali naye, Wala usiukaribie mlango wa nyumba yake.
9 Usije ukawapa wengine heshima yako, Na wakorofi miaka yako;
10 Wageni wasije wakashiba nguvu zako; Kazi zako zikawa ndani ya nyumba ya mgeni;
11 Nawe ukaziombolea siku zako za mwisho, Nyama yako na mwili wako utakapoangamia;
12 Ukasema, Jinsi nilivyochukia maonyo, Na moyo wangu ukadharau kukemewa;
13 Wala sikuisikia sauti ya waalimu wangu, Wala sikuwategea sikio langu walionifundisha!
14 Nalikuwa karibu na kuingia katika maovu yote, Katikati ya mkutano na kusanyiko.
15 Unywe maji ya birika lako mwenyewe, Na maji yenye kububujika katika kisima chako.
16 Je! Chemchemi zako zitawanyike mbali, Na mito ya maji katika njia kuu?
17 Yawe yako mwenyewe peke yako, Wala si ya wageni pamoja nawe.
18 Chemchemi yako ibarikiwe; Nawe umfurahie mke wa ujana wako.
19 Ni ayala apendaye na paa apendezaye; Maziwa yake yakutoshe sikuzote; Na kwa upendo wake ushangilie daima.
20 Mwanangu! Mbona unashangilia malaya, Na kukikumbatia kifua cha mgeni?
21 Kwa maana njia za mwanadamu zi mbele za macho ya Bwana, Na mienendo yake yote huitafakari.
22 Maovu yake yeye yatampata mdhalimu, Naye atashikwa kwa kamba za dhambi zake.
23 Atakufa huyo kwa kukosa maonyo, Naye atapotea kwa wingi wa ujinga wake.

Introduction de la Bible en Swahili de l’est

Verset liés

L'outil de verset lié est un instrument précieux qui ouvre des horizons nouveaux dans l'étude biblique. En reliant les versets apparentés au sein des Écritures, cet outil permet aux chercheurs et aux étudiants de la Bible d'explorer les thèmes, les concepts et les enseignements clés à travers différents livres bibliques. Grâce à la fonctionnalité de verset lié, nous pouvons établir des connexions profondes entre les passages, obtenir une compréhension contextuelle plus profonde et saisir la cohérence et la richesse des enseignements bibliques dans leur ensemble. Que ce soit pour des études personnelles, des enseignements ou des recherches plus poussées, l'outil de verset lié s'avère être un compagnon précieux qui enrichit notre exploration des vérités bibliques et renforce notre compréhension globale des Écritures saintes.