Proverbes 12
Versets liés

1 Kila apendaye mafundisho hupenda maarifa; Bali yeye achukiaye kulaumiwa ni kama mnyama.
2 Mtu mwema atapata upendeleo kwa Bwana; Bali mtu wa hila atahukumiwa naye.
3 Mtu hatathibitika kwa njia ya uovu; Shina la mwenye haki halitaondolewa kamwe.
4 Mwanamke mwema ni taji ya mumewe; Bali aaibishaye ni kama kuoza mifupani mwake.
5 Mawazo ya mwenye haki ni adili; Bali mashauri ya mtu mwovu ni hadaa.
6 Maneno ya waovu huotea damu; Bali kinywa cha wanyofu kitawaokoa.
7 Waovu huangamia, hata hawako tena; Bali nyumba ya mwenye haki itasimama.
8 Mtu atasifiwa kwa kadiri ya akili zake; Bali mwenye moyo wa ukaidi atadharauliwa.
9 Afadhali mtu anayedharauliwa, ikiwa ana mtumwa, Kuliko ajisifuye, ikiwa anahitaji chakula.
10 Mwenye haki huufikiri uhai wa mnyama wake; Bali huruma za mtu mwovu ni ukatili.
11 Alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele; Bali afuataye mambo ya upuzi hana ufahamu.
12 Asiye haki hutamani nyavu za wabaya; Bali shina lao wenye haki huleta matunda.
13 Katika kosa la midomo kuna mtego kwa mbaya; Bali mwenye haki atatoka katika taabu.
14 Mtu atashiba mema kwa matunda ya kinywa chake; Na atarudishiwa matendo ya mikono yake.

Le fou et le sage

15 Njia ya mpumbavu imenyoka machoni pake mwenyewe; Bali yeye aliye na hekima husikiliza shauri.
16 Ghadhabu ya mpumbavu hujulika mara; Bali mtu mwerevu husitiri aibu.
17 Atamkaye maneno ya kweli hufunua haki; Bali shahidi wa uongo hutamka hila.
18 Kuna anenaye bila kufikiri, kama kuchoma kwa upanga; Bali ulimi wa mwenye haki ni afya.
19 Mdomo wa kweli utathibitishwa milele; Bali ulimi wa uongo ni wa kitambo tu.
20 Hila imo mioyoni mwao wafikirio uovu; Bali wafanyao mashauri ya amani, kwao kuna furaha.
21 Mwenye haki hatapatikana na msiba wo wote; Bali wasio haki watajazwa mabaya.
22 Midomo ya uongo ni chukizo kwa Bwana; Bali watendao uaminifu ndio furaha yake.
23 Mwanadamu mwenye busara husitiri maarifa; Bali moyo wa wapumbavu hutangaza upumbavu.
24 Mkono wa mwenye bidii utatawala; Bali mvivu atalipishwa kodi.
25 Uzito katika moyo wa mtu huuinamisha; Bali neno jema huufurahisha.
26 Mwenye haki ni kiongozi cha mwenzake; Bali njia ya wasio haki huwakosesha.
27 Mtu mvivu hapiki mawindo yake; Bali mwenye bidii anazo mali za thamani.
28 Katika njia ya haki kuna uhai; Wala hakuna mauti katika mapito yake.

Introduction de la Bible en Swahili de l’est

Verset liés

L'outil de verset lié est un instrument précieux qui ouvre des horizons nouveaux dans l'étude biblique. En reliant les versets apparentés au sein des Écritures, cet outil permet aux chercheurs et aux étudiants de la Bible d'explorer les thèmes, les concepts et les enseignements clés à travers différents livres bibliques. Grâce à la fonctionnalité de verset lié, nous pouvons établir des connexions profondes entre les passages, obtenir une compréhension contextuelle plus profonde et saisir la cohérence et la richesse des enseignements bibliques dans leur ensemble. Que ce soit pour des études personnelles, des enseignements ou des recherches plus poussées, l'outil de verset lié s'avère être un compagnon précieux qui enrichit notre exploration des vérités bibliques et renforce notre compréhension globale des Écritures saintes.