Psaumes 77
Versets liés

Les hauts faits de Dieu dans le passé

1 Nimpazie Mungu sauti yangu, Naam, nimpazie Mungu, naye atanisikia.
2 Siku ya taabu yangu nalimtafuta Bwana; Mkono wangu ulinyoshwa usiku, haukulegea; Nafsi yangu ilikataa kufarijika.
3 Nilipotaka kumkumbuka Mungu nalifadhaika; Nilipotaka kutafakari roho yangu ilizimia.
4 Ulizishika kope za macho yangu zisifumbike; Naliona mashaka nisiweze kunena.
5 Nalifikiri habari za siku za kale, Miaka ya zamani zilizopita.
6 Nakumbuka wimbo wangu usiku, Nawaza moyoni mwangu, Roho yangu ikatafuta.
7 Je! Bwana atatupa milele na milele? Hatatenda fadhili tena kabisa?
8 Rehema zake zimekoma hata milele? Ahadi yake imekwisha hata vizazi vyote?
9 Mungu amesahau fadhili zake? Amezuia kwa hasira rehema zake?
10 Nikasema, Ndio udhaifu wangu huo; Lakini nitaikumbuka miaka ya mkono wa kuume wake Aliye juu.
11 Nitayakumbuka matendo ya Bwana; Naam, nitayakumbuka maajabu yako ya kale.
12 Pia nitaitafakari kazi yako yote; Nitaziwaza habari za matendo yako.
13 Ee Mungu, njia yako i katika utakatifu; Ni nani aliye mungu mkuu kama Mungu?
14 Wewe ndiwe Mungu ufanyaye maajabu; Uliudhihirisha uweza wako kati ya mataifa.
15 Kwa mkono wako umewakomboa watu wako, Wana wa Yakobo na Yusufu.
16 Ee Mungu, yale maji yalikuona, Yale maji yalikuona, yakaogopa. Vilindi vya maji navyo vikatetemeka,
17 Mawingu yakamwaga maji. Mbingu nazo zikatoa sauti, Mishale yako nayo ikatapakaa.
18 Sauti ya radi yako ikawa katika kisulisuli; Umeme uliuangaza ulimwengu. Nchi ilitetemeka na kutikisika;
19 Njia yako ilikuwa katika bahari. Na mapito yako yalikuwa katika maji makuu; Hatua zako hazikujulikana.
20 Uliwaongoza watu wako kama kundi, Kwa mkono wa Musa na Haruni.

Introduction de la Bible en Swahili de l’est

Verset liés

L'outil de verset lié est un instrument précieux qui ouvre des horizons nouveaux dans l'étude biblique. En reliant les versets apparentés au sein des Écritures, cet outil permet aux chercheurs et aux étudiants de la Bible d'explorer les thèmes, les concepts et les enseignements clés à travers différents livres bibliques. Grâce à la fonctionnalité de verset lié, nous pouvons établir des connexions profondes entre les passages, obtenir une compréhension contextuelle plus profonde et saisir la cohérence et la richesse des enseignements bibliques dans leur ensemble. Que ce soit pour des études personnelles, des enseignements ou des recherches plus poussées, l'outil de verset lié s'avère être un compagnon précieux qui enrichit notre exploration des vérités bibliques et renforce notre compréhension globale des Écritures saintes.