Psaumes 75
Versets liés

Dieu, le juge souverain

1 Ee Mungu, twakushukuru. Twakushukuru kwa kuwa Jina lako li karibu; Watu huyasimulia matendo yako ya ajabu.
2 Nitakapoufikia wakati ulioamriwa, Mimi nitahukumu hukumu za haki.
3 Ingawa dunia na wote wakaao humo wataharuki, Mimi mwenyewe nimezisimamisha nguzo zake.
4 Naliwaambia waliojivuna, Msijivune; Na wasio haki, Msiiinue pembe.
5 Msiiinue pembe yenu juu, Wala msinene kwa shingo ya kiburi.
6 Maana siko mashariki wala magharibi, Wala nyikani itokako heshima.
7 Bali Mungu ndiye ahukumuye; Humdhili huyu na kumwinua huyu.
8 Maana mkononi mwa Bwana mna kikombe, Na mvinyo yake inatoka povu; Kumejaa machanganyiko; Naye huyamimina. Na sira zake wasio haki wa dunia Watazifyonza na kuzinywa.
9 Bali mimi nitatangaza matendo yako milele, Nitamwimbia Mungu wa Yakobo.
10 Pembe zote za wasio haki nitazikata, Na pembe za mwenye haki zitainuka.

Introduction de la Bible en Swahili de l’est

Verset liés

L'outil de verset lié est un instrument précieux qui ouvre des horizons nouveaux dans l'étude biblique. En reliant les versets apparentés au sein des Écritures, cet outil permet aux chercheurs et aux étudiants de la Bible d'explorer les thèmes, les concepts et les enseignements clés à travers différents livres bibliques. Grâce à la fonctionnalité de verset lié, nous pouvons établir des connexions profondes entre les passages, obtenir une compréhension contextuelle plus profonde et saisir la cohérence et la richesse des enseignements bibliques dans leur ensemble. Que ce soit pour des études personnelles, des enseignements ou des recherches plus poussées, l'outil de verset lié s'avère être un compagnon précieux qui enrichit notre exploration des vérités bibliques et renforce notre compréhension globale des Écritures saintes.