Psaumes 44
Versets liés

Prière d’Israël opprimé

1 Ee Mungu, tumesikia kwa masikio yetu Baba zetu wametuambia, Matendo uliyoyatenda siku zao, siku za kale.
2 Wewe kwa mkono wako uliwafukuza mataifa, Ukawakalisha wao. Wewe uliwatesa watu wa nchi, Ukawaeneza wao.
3 Maana si kwa upanga wao walivyoimiliki nchi, Wala si mkono wao uliowaokoa; Bali mkono wako wa kuume, naam, mkono wako, Na nuru ya uso wako, kwa kuwa uliwaridhia.
4 Ee Mungu, Wewe ndiwe mfalme wangu, Uagize mambo ya wokovu kwa Yakobo.
5 Kwa nguvu zako tutawaangusha watesi wetu; Kwa jina lako tutawakanyaga watupingao.
6 Maana sitautumainia upinde wangu, Wala upanga wangu hautaniokoa.
7 Bali Wewe ndiwe uliyetuokoa na watesi wetu; Na watuchukiao umewaaibisha.
8 Tumejisifia Mungu mchana kutwa, Na jina lako tutalishukuru milele.
9 Lakini umetutupa, umetufedhehesha, Wala hutoki na majeshi yetu.
10 Waturudisha nyuma tukampa mtesi kisogo, Na watuchukiao wanajipatia mateka.
11 Umetutoa kama kondoo tuwe chakula, Na kututawanya kati ya mataifa.
12 Wawauza watu wako bila kupata mali, Wala hukupata faida kwa thamani yao.
13 Umetufanya kuwa lawama kwa jirani zetu, Mzaha na dhihaka kwao wanaotuzunguka.
14 Umetufanya kuwa mithali kwa mataifa, Sababu ya kutikisa kichwa kwa watu wa nchi.
15 Mchana kutwa fedheha yangu i mbele yangu, Na haya ya uso wangu imenifunika,
16 Kwa sauti ya mwenye kulaumu na kukufuru, Kwa sababu ya adui na mjilipiza kisasi.
17 Haya yote yametupata, bali hatukukusahau, Wala hatukulihalifu agano lako.
18 Hatukuiacha mioyo yetu irudi nyuma, Wala hatua zetu hazikuiacha njia yako.
19 Hata utuponde katika kao la mbwa-mwitu, Na kutufunika kwa uvuli wa mauti.
20 Ikiwa tumelisahau jina la Mungu wetu, Au kumnyoshea mungu mgeni mikono yetu;
21 Je! Mungu hatalichunguza neno hilo? Maana ndiye azijuaye siri za moyo.
22 Hasha! Kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa; Tunafanywa kondoo waendao kuchinjwa.
23 Amka, Bwana, mbona umelala? Ondoka, usitutupe kabisa.
24 Mbona unatuficha uso wako, Na kusahau kuonewa na kudhulumiwa kwetu?
25 Maana nafsi yetu imeinama mavumbini, Tumbo letu limegandamana na nchi.
26 Uondoke, uwe msaada wetu, Utukomboe kwa ajili ya fadhili zako.

Introduction de la Bible en Swahili de l’est

Verset liés

L'outil de verset lié est un instrument précieux qui ouvre des horizons nouveaux dans l'étude biblique. En reliant les versets apparentés au sein des Écritures, cet outil permet aux chercheurs et aux étudiants de la Bible d'explorer les thèmes, les concepts et les enseignements clés à travers différents livres bibliques. Grâce à la fonctionnalité de verset lié, nous pouvons établir des connexions profondes entre les passages, obtenir une compréhension contextuelle plus profonde et saisir la cohérence et la richesse des enseignements bibliques dans leur ensemble. Que ce soit pour des études personnelles, des enseignements ou des recherches plus poussées, l'outil de verset lié s'avère être un compagnon précieux qui enrichit notre exploration des vérités bibliques et renforce notre compréhension globale des Écritures saintes.