Théo place, étudier sérieusement la parole
Tous droits réservés
© Théo place - 2023

Psaumes 136
Versets liés

La bonté éternelle de Dieu

1 Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
2 Mshukuruni Mungu wa miungu; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
3 Mshukuruni Bwana wa mabwana; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
4 Yeye peke yake afanya maajabu makuu; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
5 Yeye aliyefanya mbingu kwa fahamu zake; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
6 Yeye aliyeitandaza nchi juu ya maji; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
7 Yeye aliyefanya mianga mikubwa; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
8 Jua litawale mchana; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
9 Mwezi na nyota zitawale usiku; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
10 Yeye aliyewapiga Wamisri kwa kuwaua wazaliwa wa kwanza wao; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
11 Akawatoa Waisraeli katikati yao; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
12 Kwa mkono hodari na mkono ulionyoshwa; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
13 Yeye aliyeigawa Bahari ya Shamu; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
14 Akawavusha Israeli katikati yake; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
15 Akamwangusha Farao na jeshi lake katika Bahari ya Shamu; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
16 Yeye aliyewaongoza watu wake jangwani; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
17 Yeye aliyewapiga wafalme wakuu; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
18 Akawaua wafalme mashuhuri; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
19 Sihoni, mfalme wa Waamori; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
20 Na Ogu, mfalme wa Bashani; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
21 Akaitoa nchi yao iwe urithi; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
22 Urithi wa Israeli mtumishi wake; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
23 Aliyetukumbuka katika unyonge wetu; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
24 Akatuokoa na watesi wetu; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
25 Kila chenye mwili akipa chakula chake; Kwa maana fadhili zake ni za milele.
26 Mshukuruni Mungu wa mbingu; Kwa maana fadhili zake ni za milele.

Introduction de la Bible en Swahili de l’est

Verset liés

L'outil de verset lié est un instrument précieux qui ouvre des horizons nouveaux dans l'étude biblique. En reliant les versets apparentés au sein des Écritures, cet outil permet aux chercheurs et aux étudiants de la Bible d'explorer les thèmes, les concepts et les enseignements clés à travers différents livres bibliques. Grâce à la fonctionnalité de verset lié, nous pouvons établir des connexions profondes entre les passages, obtenir une compréhension contextuelle plus profonde et saisir la cohérence et la richesse des enseignements bibliques dans leur ensemble. Que ce soit pour des études personnelles, des enseignements ou des recherches plus poussées, l'outil de verset lié s'avère être un compagnon précieux qui enrichit notre exploration des vérités bibliques et renforce notre compréhension globale des Écritures saintes.