1 Chroniques 8
Versets liés

Descendants de Benjamin établis à Jérusalem

1 Naye Benyamini akamzaa Bela, mzaliwa wake wa kwanza, na wa pili Ashbeli, na wa tatu Ahiramu;
2 na wa nne Noha, na wa tano Rafa.
3 Na Bela alikuwa na wana; Adari, na Gera, na Abihudi;
4 na Abishua, na Naamani, na Ahoa;
5 na Gera, na Shufamu, na Huramu.
6 Na hawa ndio wana wa Ehudi. (Hao ndio wakuu wa mbari za baba zao miongoni mwa wenyeji wa Geba; nao wakawachukua mateka mpaka Manahathi;
7 na Naamani, na Ahoa, na Gera; aliwachukua mateka). Naye akamzaa Uza, na Ahihudi.
8 Na Shaharaimu akazaa watoto katika Bara-Moabu, baada ya kuwafukuza wakeze Hushimu na Baara.
9 Akazaliwa na Hodeshi, mkewe; Yobabu, na Sibia, na Mesha, na Malkamu;
10 na Yeusi, na Shakia, na Mirma. Hao ndio wanawe, wakuu wa mbari za baba zao.
11 Naye alikuwa amezaliwa na Hushimu, Abitubu, na Elpaali.
12 Na wana wa Elpaali; Eberi, na Mishamu, na Shemedi, ambaye ndiye aliyejenga Ono na Lodi, pamoja na vijiji vyake;
13 na Beria, na Shema, waliokuwa wakuu wa mbari za baba zao miongoni mwa wenyeji wa Aiyaloni, wale ambao waliwakimbiza wenyeji wa Gathi.
14 Na Ahio, na Ghashaki, na Yeremothi;
15 na Zebadia, na Aradi, na Ederi;
16 na Mikaeli, na Ishpa, na Yoha; walikuwa wana wa Beria.
17 Na Zebadia, na Meshulamu, na Hizki, na Heberi;
18 na Ishmerai, na Izlia, na Yobabu; walikuwa wana wa Elpaali.
19 Na Yakimu, na Zikri, na Zabdi;
20 na Elienai, na Silethai, na Elieli;
21 na Adaya, na Beraya, na Shimrathi; walikuwa wana wa Shema.
22 Na Ishpani, na Eberi, na Elieli;
23 na Abdoni, na Zikri, na Hanani;
24 na Hanania, na Elamu, na Anthothiya;
25 na Ifdeya, na Penueli; walikuwa wana wa Shashaki.
26 Na Shamsherai, na Sheharia, na Athalia;
27 na Yaareshia, na Eliya, na Zikri; walikuwa wana wa Yerohamu.
28 Hao ndio waliokuwa wakuu wa mbari za baba zao, katika vizazi vyao vyote, watu maarufu; na hao walikuwa wakikaa Yerusalemu.
29 Basi huko Gibea alikaa babaye Gibea, jina lake Yeieli, ambaye jina la mkewe aliitwa Maaka;
30 na mwanawe, mzaliwa wake wa kwanza, alikuwa Abdoni, na Suri, na Kishi, na Baali, na Nadabu;
31 na Gedori, na Ahio, na Zekaria
32 Na Miklothi akamzaa Shimea. Na hao nao walikuwa wakikaa pamoja na ndugu zao huko Yerusalemu, kuwakabili ndugu zao.
33 Naye Neri akamzaa Kishi; na Kishi akamzaa Sauli; na Sauli akamzaa Yonathani, na Malkishua, na Abinadabu, na Eshbaali.
34 Na mwanawe Yonathani alikuwa Meribaali; na Meribaali akamzaa Mika.
35 Na wana wa Mika; Pithoni, na Meleki, na Tarea, na Ahazi.
36 Na Ahazi akamzaa Yara; na Yara akamzaa Alemethi, na Azmawethi, na Zimri; na Zimri akamzaa Mosa;
37 na Mosa akamzaa Binea; na mwanawe huyo alikuwa Refaya, na mwanawe huyo ni Ekasa, na mwanawe huyo ni Aseli;
38 naye Aseli alikuwa na wana sita, ambao majina yao ni haya; Azrikamu, na Bokeru, na Ishmaeli, na Shearia, na Obadia, na Hanani. Hao wote walikuwa wana wa Aseli.
39 Na wana wa Esheki nduguye ni hawa; mzaliwa wake wa kwanza, Ulamu, na wa pili Yeushi, na wa tatu Elifeleti.
40 Na wana wa Ulamu walikuwa watu hodari wa vita, wapiga upinde, nao walikuwa na wana wengi, na wana wa wana, watu mia na hamsini. Hao wote ndio waliokuwa wana wa Benyamini.

Introduction de la Bible en Swahili de l’est

Verset liés

L'outil de verset lié est un instrument précieux qui ouvre des horizons nouveaux dans l'étude biblique. En reliant les versets apparentés au sein des Écritures, cet outil permet aux chercheurs et aux étudiants de la Bible d'explorer les thèmes, les concepts et les enseignements clés à travers différents livres bibliques. Grâce à la fonctionnalité de verset lié, nous pouvons établir des connexions profondes entre les passages, obtenir une compréhension contextuelle plus profonde et saisir la cohérence et la richesse des enseignements bibliques dans leur ensemble. Que ce soit pour des études personnelles, des enseignements ou des recherches plus poussées, l'outil de verset lié s'avère être un compagnon précieux qui enrichit notre exploration des vérités bibliques et renforce notre compréhension globale des Écritures saintes.